Haruni Sanchawa na Makongoro Oging'
LISEMWALO lipo na kama halipo laja! Usemi huu umekamilika pale
Charles Wilbroad alipopata pigo la kumpoteza mtoto wake kipenzi,
Emmanuel Charles (7), siku ambayo gazeti hili liliandika habari
kuhusiana na siri za Freemasons zilizotolewa na kijana huyo.
Akizungumza na gazeti hili, Charles alisema baada ya kuzungumza na
mwandishi wetu kuhusiana na siri za Freemasons na kueleza jinsi
alivyotakiwa amtoe kafara mwanaye, mtoto huyo alifariki dunia siku
gazeti hili lilipokuwa mtaani.
“Mwanangu alifariki ghafla baada ya
kuugua kwa saa mbili mfululizo kuanzia saa 1:00 asubuhi hadi saa 3:00,
Jumanne ya Juni 26, mwaka huu. Madaktari walieleza kuwa kifo chake
kimesababishwa na kuishiwa damu mwilini,” alisema Wilbroad.
Wilbroad
aliendelea kusema kuwa kifo cha mwanaye kilimshtua sana kwani aliugua
na kufa ghafla, hali aliyoitafsiri kuwa huenda ilisababishwa na imani
yake ya Freemasons.
“Alianza kuumwa saa moja asubuhi, akaanguka na
kupoteza fahamu. Tukamkimbiza hospitalini lakini ilipofika saa tatu
asubuhi, alikata roho. Wamemnyonya damu mwanangu kwa sababu madaktari
walisema ameishiwa damu,” alisema Wilbroad na kufafanua kuwa kifo hicho
kiliwashitua wengi waliokuwa wakimfahamu mtoto wake huyo.
Awali,
Wilbroad aliliambia gazeti hili kuwa aliwahi kuambiwa amtoe kafara mtoto
wake huyo kimazingara ili maisha yake yawe mazuri lakini alikataa,
badala yake akaenda kuvitupa baharini vitu alivyopewa kufanyia
ushirikina huo baada ya kushindwa masharti.
Alivitaja vitu hivyo
ambavyo alipewa na mtu mmoja ambaye anaishi Uarabuni (Dubai) mwaka 2009
kuwa ni pamoja na mkufu, pete pamoja na fomu maalum aliyoijaza ambayo
ilieleza pamoja na mambo mengine kwamba akifa, mrithi wake angekuwa
mtoto wake aitwaye Emanuel ambaye sasa ni marehemu.
Maziko ya kijana Emmanuel yalifanyika katika Kata ya Nyamililo, Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza Juni 27, mwaka huu.
No comments:
Post a Comment