Makamu
Mwenyekiti wa Simba, Godfrey Nyange ‘Kaburu’ (wa pili kushoto) akiongea
na wanahabari (hawapo pichani) muda mfupi kabla ya kupokea hawala hiyo.
Kaburu
akipokea hawala hiyo kutoka kwa Mkurugenzi wa Sheria wa TBL, Kelvin
Kilindo, wanaoshuhudia kushoto ni Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala
na Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, George Kavishe.
Kilindo akiwashukuru wote waliofika kwenye mkutano huo.
Kaburu akiishukuru TBL kwa msaada wao na watu waliohudhuria mkutano huo.
KAMPUNI ya Tanzania Breweries (TBL) kupitia bia yake ya Kilimanjaro,
leo imeikabidhi klabu ya Simba, hawala ya shilingi milioni 20, kwa
ajili ya kufanikisha mkutano wake mkuu unaotarajiwa kufanyika Agosti, 5
mwaka huu. Makabidhiano hayo yamefanyika makao makuu ya TBL, Ilala,
Mchikichini jijini Dar es Salaam
No comments:
Post a Comment