Kyle Glover ambae ni mtoto wa mke
wa zamani wa Mwimbaji Usher Raymond, amefariki dunia leo kutokana na
kuumia kwenye ajali ya pikipiki za kwenye maji maarufu kama Jetski
mwanzoni mwa mwezi huu huko Georgia Marekani.
Madaktari
wametoa mashine zilizokua zinasaidia kumuweka hai mtoto huyo aliekua na
umri wa miaka 11 baada ya kugundua kwamba majeraha aliyoyapata
yasingeweza kutibika.
Kyle akiwa
na rafiki yake wa kike mwenye umri wa miaka 15 walipata ajali july 8
2012 huko Georgia baada ya Inner tube waliyokuwemo iliyokua ikivutwa na
boti kugongwa na Jetski wakiwa kwenye maji na hivyo kupata majeraha ya
kichwa.
No comments:
Post a Comment